Trump ataka mabomu mapya ya atomiki kupamba na Urusi
Jeshi la Marekani litaimarisha silaha zake za kinyuklia pamoja na kutengeneza mabomu mapya ya atomiki yenye nguvu ndogo, huku ikiwa inaitupia jicho Urusi, kulingana na sera mpya iliyotangazwa jana kwenye taarifa ya Wizara ya Ulinzi ya Marekani Pentagon.
Juhudi hizo katika kuimarisha silaha za kinyuklia ni mabadiliko makubwa kutoka wakati wa uongozi wa Rais Barack Obama, aliyetoa wito wa kuondoa silaha za kinyuklia katika hotuba yake mjini Pargue mwaka 2009.
Wizara ya ulinzi ya Marekani Pentagon ina wasiwasi kwamba Urusi inaamini mabomu ya kawaida ya atomiki ya Marekani ni makubwa sana kiasi ya kwamba hayawezi kutumika, kutoaka na kwamba yakitumika yanaweza kusababisha kisasi pamoja na uharibifu mkubwa ulimwengun

Comments
Post a Comment