Mwana wa Fidel Castro 'ajitoa uhai'

Mwana wa mwanamapinduzi wa Cuba Fidel Castro, Fidel Ángel Castro Díaz-Balart, mwenye umri wa miaka 68 amejiua akiwa mji mkuu wa Havana, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya serikali nchini Cuba vimetangaza.
Alipatikana akiwa amefariki Alhamisi asubuhi, na inadaiwa kwamba alikuwa anatatizwa na msongo wa mawazo.
Castro Díaz-Balart alifahamika sana kama "Fidelito" na alikuwa kifungua mimba wa rais huyo wa zamani wa Cuba aliyefariki dunia Novemba 2016.
Alifanya kazi kama mwanafizikia ya nyuklia, baada ya kupokea mafunzo katika uliokuwa Muungano wa Usovieti.

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.