Wizara ya omba radhi

Wizara ya Ujenzi, uchukuzi na Mawasiliano kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme, wameomba radhi wananchi wanaotumia kivuko cha Mv Magogoni jijini Dar es salaam, kuwa na subira katika kipindiki hiki ambacho wanashughulikia tatizo lake.
Kwenye taarifa maalum iliyotolewa kwa vyombo vya habari, imesema kivuko hicho kimeharibika kutokana na kamba na nanga za maboti ya wavuvi kunasa kwenye mitambo ya kuendesa kivuko hiko, na kusababisha huduma kusimama kwa muda.
Kutokana na tatizo hilo Wizara imesema viuko vingine kama Mv. Kazi na Mv. Kigamboni vinaendelea na shughuli za kuvusha watu, huku ikiwataka wananchi wanaofanya shughuli zao za kibinadamu upande wa Kigamboni kutokufanya shughuli hizo karibu na maegesho ya kivuko ili kuzuia tukio kama hilo kujitokeza tena.

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.