Wito umetolewa kwa wanaume kujenga utamaduni wa kuwasindikiza wake zao kwenda kiliniki ili kuendana na sera ya afya ya uzazi kitaifa inayomtaka baba kushiriki katika kiliniki ya mama na mtoto wakati wote wa ujauzito mapaka kujifungua.





ISAAC ARON ISAAC
KIGOMA:
Wito umetolewa kwa wanaume kujenga utamaduni wa kuwasindikiza wake zao kwenda kiliniki ili kuendana na sera ya afya ya uzazi kitaifa inayomtaka baba kushiriki katika kiliniki ya  mama na mtoto wakati wote wa ujauzito mapaka kujifungua.

miongoni mwa akina baba ambao wameunga mkono sera ya afya ya kushiriki kliniki ni Fedrick Joseph mkazi wa wilaya ya kasulu mkoa wa kigoma amesema kuwa swala la afya ni mhimu sana huku wakiwataka akina baba kulinda afya ya wake zao hasa kushiriki katika kiliniki ya mama, baba na mtoto.

Na kwaupande wake Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Nyanyunsi Wilayani kasulu DKT Tobiasi Sigwejo amesema kuwa kila mwanaume anatakiwa kuambatana na mke wake ili kujua afya yake ingwa bado Elimu ni kidogo sana miongoni mwa jamii jambo linalokwamisha mpango wa kiliniki ya baba, mama na mtoto.

Bado akina mama wanapaswa kuelewa kuwa afya ytake ni muhimu sana katika kujenga Tanzania ya kesho hasa tunapo itaji kupiga hatua za kimaendeleo,kwa hiyo sera ya afya ipo kwaajili ya maendeleo ya mtanzania mmoja mmoja.

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.