Waliotoka jera kwa msamaha wa Rais kufungwa tena
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Jijini Dar es salaam Lazaro Mambosasa, amesema wahalifu waliotoka jela kwa msamaha wa Rais hawatasita kuwarudisha tena jela iwapo wataendelea na tabia za uhalifu.

Kamanda Mambosasa ametoa kauli hiyo leo alipokuwa akizungumza na waandihsi wa habari alipokuwa akiwapa taarifa za uhalifu, na kusema kwamba watu wanaoongoza kwa vitendo vya uhalifu ni wale waliotoka kwa msamaha wa Rais, na kwamba wanatumwa na wenzao walio jela.
Akiendelea kuzungumzia suala hilo Kamanda Mambosasa amesema watu hao wamekuwa wakirudia maeneo walioficha silaha kabla hawajakamata na kufungwa, na kuzichukua kuzitumia kwenye matukio ya uhalifu, huku wakendelea kuwasiliana na wale ambao bado wako gerezani kujua wameweka wapi silaha ili kuzitumia kwenye kazi zao, na kisha kuwapelekea posho.
Comments
Post a Comment