Wakulima wa zao la Tumbaku wa Chama Cha Msingi Cha Ukonongo katika halmashauri ya Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi wamelalamikia kucheleweshewa malipo

 

Katavi:

Wakulima wa zao la Tumbaku wa Chama Cha Msingi Cha Ukonongo katika halmashauri ya Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi wamelalamikia kucheleweshewa malipo ya zao la tumbaku katika msimu wa mwaka uliopita.

Wakizungumza na Mpanda redio kwa nyakati tofauti wamesema licha ya mchanganuo wa malipo kufanyika bado wakulima wengi hawajapatiwa fedha zao hali ambayoinasababisha ugumu wamaisha katika msimu huu wa kilimo .

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama hicho cha msingi Godfley Malilo amesema changamoto iliyopo ni uingizwaji wa ushuru wa chama umecheleweshwa lakini hatua za kuanza malipo hayo yanatarajiwa kuaanza wiki ijayo.

Chama hicho cha msingi kinawakulima wa tumbaku zaidi ya elfu mbili na kimekuwa kikichangia kwa kiasi kikubwa katika pato la halimshauri ya wilaya ya Mlele.
Source Paul mathius
Editor Alinanuswe Edward.

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.