WAKULIMA MPANDA/ KATAVI WAITAKA SERIKALI KUTENGANISHA MAENEO YA WAFUGAJI NA WAKULIMA



Baadhi ya wakazi wa kata ya Magamba Manispa ya Mpanda mkoani Katavi wameitaka serikali kutenga maeneo ya wafugaji na wakulima ili kuepusha migogoro ya ardhi inayojitokeza mara kwa mara
Wakizungumza na Mpanda Radio kwa nyakati tofauti wananchi hao wamesema wakulima na wafugaji wanapoendesha shughuli zao katika eneo moja huchangia mifarakano isiyo ya lazima na kushauri wafugaji kutengewa eneo tofauti na wakulima ili kuondoa mwingiliano

Kwa upande wake Bi Anna Thomas ambaye ni mwenyekiti wa serikali za mitaa amekiri kuwepo kwa migogoro ya mara kwa mara baina ya wakulima na wafugaji na kuongeza kuwa inachangangiwa na wafugaji kuwa na mifugo mengi kwenye eneo dogo

Philemone Tesha Afisa kilimo wa kata ya magamba amesema serikali ina mpango wa kutenga maeneo ya kuchungia yatakayokuwa tofauti na mashamba japo hakubainisha wazi mpango huo ni lini utaanza kutekelezwa

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.