Utekelezaji wa agizo la Wizara ya Elimu kuweka kiwango sawa cha ufaulu kwa shule za binafsi na serikali, umekuwa kaa la moto.



MPANDA
Walimu wa shule za sekondari za binafsi mkoani Katavi wameelezea kuwepo kwa  changamoto utekelezaji wa agizo la kuweka kiwango sawa cha ufaulu kwa shule za binafsi na serikali.

Kauli hiyo inakuja kutokana na maagizo ya serikali kupitia wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi ambapo shule binafsi zimetakiwa kubadilisha mfumo kwa ufaulu wa wanafunzi na kuwa sawa na shule za serikali.
Wamesema itawalazimu kubadilika japo hatua hiyo haitamjenga mwanafunzi kitaaluma kwani wengi wao wanaosomea katika shule binafsi ni wale walioshindwa kufaulu kwenye shule za serikali.

Hatua hiyo ya wizara ya elimu imetajwa kuwa ni moja ya kupunguza upatikanaji wa wanafunzi watakao jiunga na shule binafsi  kwani kutakuwa hakuna umuhimu kutokana na usawa katika viwango vya ufaulu.
Source Esther Baraka
Editor Aliananuswe Edward               

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.