Tanzania, Msumbiji watiliana sain





Tanzania na Msumbiji leo zimekubaliana kuendesha msako wa pamoja dhidi ya makundi ya wahalifu ikiwemo wale wanaojihusisha na vitendo vya ujangili katika maeneo ya mipakani.


Akizungumza mara baada ya kutiliana na saini makubaliano hayo na Mkuu wa Jeshi la Polisi Msumbiji, Bernadino Rafael, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro, amesema, uamuzi huo umekuja baada ya kugundua baadhi ya wahalifu wanakimbilia nchi jirani.
Kwa upande wake IGP wa Msumbiji amesema, kuna manufaa makubwa kiulinzi na usalama kushirikiana katika kupambana na wahalifu kwa kuwa watabadilishana ujuzi kulingana na taratibu za nchi zote mbili ulivyo na kuzuia uhalifu.

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.