Takukuru yaendelea kusubiri kuwasilisha ushahidi dhidi ya Wana CCM

MWANZA

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Mkoa wa Mwanza imewaweka kiporo viongozi na makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) baada ya kuahirisha kutoa taarifa ya uchunguzi dhidi yao iliyopangwa kutolewa Januari 15.
Wanaochunguzwa kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya rushwa wakati wa mchakato wa uchaguzi ndani ya CCM ni pamoja na katibu mwenezi wa CCM Wilaya ya Ukerewe, Nicholaus Munyoro; diwani wa Kata ya Murutunguru, Musa Manka; diwani wa Kata ya Bukindo, Gabriel Gregory na Steven Mazige ambaye ni mwenyekiti wa CCM Kata ya Ukerewe.
Makada hao walitiwa mbaroni na Takukuru Desemba 2, 2017 wakati wa mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa CCM mkoani Mwanza uliofanyika katika Uwanja wa CCM Kirumba kwa madai ya kukutwa wakigawana Sh400, 000 zilizosadikiwa kuwa rushwa iliyotolewa na mmoja wa wagombea.

Akizungumza kwa njia ya simu jana kuhusu suala hilo, mkuu wa Takukuru Mkoa wa Mwanza, Ernest Makale amesema taasisi hiyo itapanga siku nyingine ya kutoa taarifa ya uchunguzi dhidi ya viongozi hao baada ya kushindwa kufanya hivyo Jumatatu iliyopita.

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.