Serikali ya Ethiopia imewakamata watu 107 kwa tuhuma za kuhusika na vurugu zilizotokea hivi karibuni katika eneo la mpaka wa mikoa ya Somali na Oromia.




ADDIS ABABA

Serikali ya Ethiopia imewakamata watu 107 kwa tuhuma za kuhusika na vurugu zilizotokea hivi karibuni katika eneo la mpaka wa mikoa ya Somali na Oromia.

Kamishna wa tume ya polisi ya Ethiopia Abiyu Assefa amesema watuhumiwa 98 kati ya hao waliokamatwa wanatokea mkoa wa Oromia na wengine tisa kutoka mkoa wa Somali.

Mapigano makali katika eneo la mpaka wa mikoa hiyo miwili yaliyotokea mwezi Septemba mwaka jana yalisababisha mapigano ya kikabila yaliyosababisha vifo vya watu kadhaa.

Mbali na vifo hivyo vinavyotajwa kutokea halikadhalika mamia ya watu walikimbia makazi yao wakihofia kuuwawa.

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.