Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli leo amemteua Mhe.Doto Mashaka Biteko kuwa Naibu Waziri wa Madini.


DAR ES SALAAM
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli leo amemteua Mhe.Doto Mashaka Biteko kuwa Naibu Waziri wa Madini.
Mhe.Biteko ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe na alikuwa Mwenyekiti wa kamati ya muda iliyochunguza madini ya Tanzanite.
Kufuatia uteuzi huo,Wizara ya Madini sasa itakuwa na Waziri na Naibu Mawaziri wawili.
Kwa mjibu wa taarifa ambayo imetolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya rais Ikulu Gerson Msigwa amesema, rais Magufuli amefanya uteuzi huu kwa lengo la kuongeza nguvu kutokana na uwingi wa majukumu katika Wizara ya Madini.

Mhe.Doto Mashaka Biteko anatarajiwa kuapishwa Jumatatu Januari 08 Januari mwaka huu Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.