Rais Magufuli kuwa Kiongozi wa kwanza barani afrika kukataa hadharani kuongezewa miaka ya kukaa madarakani.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli ameweka wazi kuwa hana mpango wowote wa kuongeza muda wa kukaa madarakani kutoka miaka 5-7 na pia hafurahishwi na mijadala hiyo.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo Januari 13 wakati alipokutana na Katibu wa Itikadi na Uenezi  IKulu, ndg. Humphrey Polepole na kumtuma awajulishe watanzania na wana CCM kwamba wapuuze mijadala hiyo kwani jambo hilo halijawahi kujadiliwa katika kikao chochote cha chama.
Kupitia taarifa iliyotlewa na Ikulu, Rais Magufuli amemuagiza Polepole kuwajulisha watanzania na wana CCM kuwa wasikubali kuyumbishwa au kupotoshwa na mambo yasiyokuwa ya msingi na badala yake wajielekeze katika kukuza uchumi na kutekeleza ilani ya CCM ya mwaka 2017.

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.