NAPE ASHITUSHWA NA MWINGILIANO WA SHUGHURI ZA KISERIKALI NA CHAMA


Mbunge wa jimbo la Mtama kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Nape Nnauye amesema kuwa kuchanganya shughuli za kijeshi na masuala ya kisiasa inaleta ukakasi kidogo lakini adai mambo kama haya yanaweza kuzungumzika. 
Nape Nnauye amesema kuwa kuna wakati inakuwa ni vigumu sana kumtofautisha Rais wa nchi na Mwenyekiti wa CCM kwa kuwa mtu huyo anakuwa ni mmoja na kwenda mbali zaidi kuwa kuna wakati huwa kuna kuwa na mvutano kati ya wanachama na viongozi wa ulinzi na usalama katika baadhi ya matukio ambayo Rais anahudhuria. 
"Bahati mbaya ni ngumu sana kumtofatisha Magufuli Rais wa Tanzania na Magufuli Mwenyekiti wa CCM kwa kuwa huyu mtu ni mmoja kwamba yeye ndiye mwenye vyeo vyote viwili lakini ni rahisi kuzitofautisha shughuli kwamba anapofanya mambo ambayo yanaihusu taasisi ya Urais ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kusichanganywe na shughuli za CCM inawezekana ikafanyika hivyo" alisema Nape Nnauye 
Aidha Nape Nnauye aliendelea kusema kuwa "Niliona katika mkutano mmoja nadhani ni Arusha pale ilikuwa ni paredi ya wanajeshi nadhani halafu baadaye nikaona shughuli za chama zimeingia, ukiangalia hapa unapata ukakasi fulani na kusema nadhani hili lina tabu ndiyo maana nasema wapi tuchore mstari wakati mwingine ndiyo inakuwa ngumu hivyo muda mwingine si suala la upendeleo bali ni wapi tuchore mstari tutofautishe shughuli za kiserikali na shughuli za chama" 

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.