MKUU WA MKOA WA TABORA AGREY MWANRI AWASAKA WAZAZI NA WALEZI AMBAO HAWAJAWAPELEKA WANAFUNZI WALIO FAULU KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA



TABORA

Serikali Mkoani Tabora imeagiza kukamatwa mara moja wazazi au walezi ambao hadi kufikia leo  Jumatatu ijayo watakuwa wameshindwa kuhakikisha kuwa watoto wao waliochaguliwa kujiunga Kidato cha kwanza mwaka huu watakuwa hawajaripoti katika Shule walizopangiwa.
Agizo hilo limetolewa mjini Sikonge na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri baada ya kupata taarifa kutoka kwa Afisa Elimu Mkoa iliyokuwa ikionyesha kuwa idadi kubwa ya wanafunzi walichaguliwa kujiunga na Kidato cha kwanza mwaka 2018 bado wengi wao hawajaripoti katika Shule walizopangiwa.
Amesema kuwa kufikia leo jumatatu  anataka kupata taarifa na majina ya wanafunzi wote waliochangiwa, na ambao hawako shuleni ikiwa  na majina ya wazazi wao ili hatua za kisheria dhidi yao ziweze kuchukuliwa kwa kosa la kumkoshesha watoto haki ya kupata elimu.
Mwanri ameongeza kuwa viongozi wa kuanzia mitaa, vitongoji, vijiji , Kata na Wilaya ni vema wahakikishe wanawatafuta watoto wote waliochaguliwa ambao hawako shuleni ili kujua walipo na wanafanya nini kwa kuwa inawezekana wapo ambao tayari wameshaozeshwa


Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.