MBUNGE VITI MAALUMU MKOA WA KATAVI KUPITIA CHADEMA ASEMA KATA YA KATUMBA H/MASHAULI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUTOKUWA NA DIWANI NI UCHELEWESHAJI WA MAENDELEO.



KATAVI:
Mbunge wa viti maalumu mkoa wa Katavi kupitia  Chadema Rhoda Kunchela amesema kitendo  cha kata ya katumba halmashauri ya Nsimbo mkoani Katavi kutokuwa na diwani ni kuchelewesha maendeleo kwa wananchi wa kata hiyo.

Hayo yamebainishwa leo na Mbunge huyo wakati akizungumza na Mpanda Radio na kusema kuwa wananchi wanakosa uwakilishi  na kushauri uchaguzi ufanyike ili apatakane diwani mwingine .

Diwani aliyekuwa akiongoza kata hiyo Mh Seneta Baraka amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela tangu mwaka uliopita  kwa kosa la kupokea rushwa.


Katika hatua nyingine Mh Kunchela  amezungumzia ziara aliyoifanya mwenyekiti wa Bawacha taifa  Halima Mdee amabye pia ni mbunge wa jimbo la kawe na kusema ziara  hiyo imefanyika mkoani katavi ikilenga kuimarisha uhai wa chama hicho.

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.