Marekani jana imetangaza kuwa itazuia kiasi cha dola milioni 65 zilizokuwa zimepangwa kulifadhili shirika la Umoja wa mataifa linalowahudumia wakimbizi wa Palestina la UNRWA, wiki mbili baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kutishia malipo ya baadaye.




WASHINGTON
Marekani jana imetangaza kuwa itazuia kiasi cha dola milioni 65 zilizokuwa zimepangwa kulifadhili shirika la Umoja wa mataifa linalowahudumia wakimbizi wa Palestina la UNRWA, wiki mbili baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kutishia malipo ya baadaye.

 Wizara hiyo imesema Marekani itatoa dola milioni 60 kati ya milioni 125 zilizopangwa awali, lakini zilizobaki zitazuiwa kwa sasa.

Maafisa wa Waziri wa Mambo ya Nje ya Marekani wamesisitiza uamuzi huo haukuchukuliwa ili kuwashinikiza viongozi wa Palestina, lakini kwa sababu Marekani inataka nchi nyingine wanachama wa Umoja wa Mataifa zisaidie kulipa na kurekebisha shirika la UNRWA.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres alisema hakuwa na taarifa ya uamuzi huo wa Marekani, lakini taarifa alizozisikia zimempa wasiwasi sana.
Source BBC
Editor Alinanuswe Edward


Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.