Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi yakili kushindwa kuandaa maadhisho ya siku ya walemavu duniani kwa miaka 2 mfululizo.



MPANDA.
Mkurugenzi wa Manspaa ya Mpanda Michael Nzyungu amekiri kutofanyika kwa maadhimisho ya siku ya walemavu duniani kwa mwaka uliopita kutokana na kutokuwa na mawasiliano ya kutosha kati ya halmashauri hiyo na ofisi ya mkoa.

Akizungumza na Mpanda Redio kwa njia ya simu Bwana Nzyungu amesema mkoa ndio wenye jukumu la kupanga sherehe  katika ngazi ya halmashauri na wilaya jambo ambalo halikufanyika.

Katika hatua nyingine  amesema kuwa suala la bajeti  sio tatizo kiasi cha kukwamisha maadhimisho hayo na kauhidi kuwa mwaka huu manispaa itahakikisha tatizo hilo halijirudii tena.

Mkoa wa katavi umeshindwa kuaandaa Maadhimisho ya siku ya walema duniani  kwa miaka miwili mfululizo ambayo hufanyika decemba tatu kila mwaka.

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.