Kuleta ndugu wa nne ili kuongezewa damu kwa tajwa kuwa kikwazo, mkoani Katavi



MPANDA

Baadhi ya Wananchi mkoani Katavi wamekitaja kitendo cha kutakiwa kuleta ndugu wanne wa kujitolea damu pindi mgonjwa anapo kuwa na tatizo la kuishiwa damu kuwa kikwazo katika  huduma ya afya .

Wamesema hayo kwa nayakati tofauti wakati wakizungumza na Mpanda radio fm na kueleza kuwa hali hiyo ndiyo inayo chochea vitendo vya rushwa ili kupata huduma.

Kwa uapande wake  mratibu  wa damu salama wa hospitali ya Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi  Khadija Juma  amesema kwa mwezi hutumika chupa 350 na inaingiza chupa 400 mpaka 600 hivyo kiwango hicho kinakidhi mahitaji ya wagonjwa.

Aidha amewaomba kujenga tabia ya  kujitolea damu kwa kwa hiari,wakati wote na siku yoyote katika masaa ya kazi.

Wiki iliyopita Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, akiwa kwenye uzinduzi wa kampeni ya kuchangia damu Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amezitaka Hospitali na vituo vya Afya nchini kuhakikisha wagonjwa hawauziwi damu.

Source Neema Manyama
Editor Alinanuswe Edward

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.