Korea Kaskazini kushiriki katika michezo ya Olimpiki nchini Korea Kusini


Korea Kaskazini imesema kuwa itatuma ujumbe wake katika michezo ya Olimpiki ya majira ya baridi 2018 inayotarajiwa kufanyika Korea Kusini mnamo mwezi Februari kulingana na mji wa Seoul.
Tangazo hilo lilijiri wakati ambapo mataifa hayo yalikutana kwa mazungumzo ya kihistoria baada ya zaidi ya miaka miwili.
Ujumbe huo utashirikisha wanariadha na mashabiki miongoni mwa wengine.
Korea Kusini pia ilipendekeza kukutanisha familia zilizotenganishwa na vita vya Korea wakati wa michezo hiyo ya majira ya baridi.
Swala hilo lina utata mkubwa miongoni mwa mataifa hayo mawili, na Korea Kusini imekuwa ikipendekeza familia ziendelee kukutanishwa.
Mpango huo wa kuzikutanisha familia unatarajiwa kufanyika wakati wa likizo ya mwaka mpya, ambayo hufanyika katikati ya michezo ya Pyeongchang.
Mji wa Seoul pia uliwataka wanariadha kutoka mataifa yote ya Korea kufanya gwaride la pamoja katika sherehe ya ufunguzi ya michezo ya Olimpiki.
Haijulikani ni vipi Korea Kaskazini ilijibu mapendekezo hayo.
Mara ya mwisho kwa mataifa yote mawili kufanya gwaride la pamoja chini ya bendera ya rasi ya Korea ni zaidi ya miaka 10 iliopita katika michezo ya olimpiki ya 2006.
Waziri wa muungano wa Korea Kusini , Cho Myoung-Gyon amesema mazungumzo hayo yanajikita zaidi katika masuala ya olimpiki lakini mambo mengine pia yatajadiliwa ikiwa ni pamoja na kutumia fursa hiyo kuimarisha uhusiano.
"Tunahudhuria mkutano huu ili kuzungumzia suala la Korea Kaskazini kushiriki katika mashindano ya Olimpiki ya msimu wa baridi yatayofanyika korea kusini na kuimarisha uhusiano wan chi hizi mbili.Ninaelewa kuwa matarajio ya wengi juu ya mkutano huu ,kwanza ni kuhusu mawasiliano baina ya nchi hizi mbili ambayo yalisitishwa kwa muda.Tuna lengo la kufanya mashindano haya ya Olimpiki kuwa ya hatua ya kwanza ya kuboresha Amani baina ya nchi hizi mbili hivyo hii ni hatua nzuri na hatuna haraka."Cho Myoung-Gyon aeleza.

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.