Chanzo cha ghasia nchini Kongo


KINSHASA:
Hasira inaonekana kuongezeka katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo dhidi ya rais Joseph Kabila tangu akatae kuondoka madarakani wakati muhula wake ulipomalizika Desemba 2016.

Rais Joseph Kabila, alifikia makubaliano na vyama vya upinzani kuandaa uchaguzi kabla ya mwisho wa mwaka 2017.

Na kufikia mwisho wa mwaka huo, rais Kabila alikuwa tayari ashafika kikomo cha utawala wake wa mihula miwili kikatiba.

Hatua ya tume ya uchaguzi kuahirisha kwa mara nyingine uchaguzi mkuu hadi Aprili mwaka 2019 baada ya kuahirisha awali hadi mwishoni mwa mwaka jana 2017 uliongeza ghadhabu iliopo.

Corneille Nangaa, kiongozi wa tume ya uchaguzi nchini, CENI, amesema ilikuwa ni muhimu kuuharisha uchaguzi huo kutokana na kuzuka ghasia katika eneo la Kasai ya kati, hali inayotatiza usajili wa wapiga kura.

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.