CHADEMA YAENDELEA KUKIMBIWA NA WANACHAMA WAKE



Wanachama 19 kutoka vyama vya upinzani katika Kata za Matambarare na Mnacho wilayani Ruangwa mkoani Lindi, wamekabidhi kadi zao kwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM).
Wanachama hao kutoka vyama vya CUF na CHADEMA, wamekabidhi kadi zao kwa Waziri wakati akizungumza na wakazi wa kijiji cha Matambarare Kusini kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini hapo.
Akiwa katika kijiji cha Matambare Kusini, Waziri Mkuu amepokea wanachama 17 ambao kati yao 13 wanatoka Chama cha Wananchi (CUF) na wanne wanatoka Chama cha Maendeleo na Demokrasia (CHADEMA). Katika kijiji cha Ng’au kata ya Mnacho, Majaliwa amepokea wanachama wawili wa (CHADEMA).




Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.