CCM ya vuna viongozi 18 wanachama wa ACT Wazalendo



MOSHI

Viongozi 18 wa chama cha ACT-Wazalendo kutoka mikoa mbalimbali nchini wamejivua nyadhifa zao na kujiunga na CCM.

Viongozi hao wamepokelewa leo Januari 17, 2018 mjini Moshi na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira ambaye hivi karibuni alihamia chama tawala. Mghwira amewahi kuwa mwenyekiti wa ACT.

Miongoni mwa wanachama hao, wapo waliokuwa wajumbe wa kamati kuu, wenyeviti wa mikoa na makatibu wa ACT.

Pia, viongozi 18 wa Chadema ngazi za kata na vijiji kutoka Wilaya ya Siha nao wamejiunga na CCM.

Akizungumzia baada ya kuwakaribisha, Polepole amesema katika kipindi cha miaka miwili ya utawala wa Serikali ya Awamu ya Tano, CCM kimeongeza wanachama zaidi ya milioni mbili.

Source Mwananchi


Editor Alianauswe Edward

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.