AFRIKA YATAKA TRUMP AOMBE RADHI KWA KUITUSI



Nchi 54 za Afrika zimemtaka Rais wa Marekani Donald Trump kuziomba radhi baada ya kuripotiwa kutumia maneno machafu alipokuwa akizungumzia kuhusu wahamiaji kutoka mataifa ya Afrika, Haiti na El Salvador wakati alipokutana na wabunge kwenye Ikulu.

 Baada ya kikao cha dharura cha mabalozi wa nchi za Afrika katika Umoja wa Mataifa, mabalozi hao wamesema wanatiwa wasiwasi na mtindo unaozidi kujitokeza kwenye utawala wa Marekani wa kuwadunisha Waafrika na kulaani vikali matamshi ya kibaguzi, ya kudunisha na ya chuki dhidi ya wageni yaliyotolewa na Rais Trump.

 Rais Donald Trump amekanusha kutumia maneno machafu juu ya nchi kadhaa ikiwa pamoja na za Afrika. Trump aliuliza kwa nini Marekani iwapokee wahamiaji kutoka nchi za uozo kama za Afrika, Haiti na El Salvador. 

Kauli ya Trump imesababisha ghadhabu na mshtuko. Umoja wa Afrika pia umemshutumu Trump kwa matamshi yake umesema umeshtushwa na umesikitishwa na umemtaka Trump aombe radhi.


Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.