34 wafariki kwa ajali ya basi



Watu 34 wamefariki na wengine 16 wamejeruhiwa na hali zao zikielezwa kuwa mbaya baada ya basi moja la abiria kugongana ana kwa ana na lori la mizigo, katika maeneo ya barabara ya Sachangwan/ Salgaa, takriban kilomita 200 kutoka mji mkuu Nairobi.
Afisa Mkuu wa idara ya polisi wa trafiki maeneo ya Bonde la Ufa, Zero Arome amesema ajali hiyo imetokea kwenye barabara kuu ya kutoka Nakuru kuelekea Eldoret Magharibi mwa Kenya.
Shirika la msalaba mwekundu nchini Kenya limeandika kwenye mtandao wake wa kijamii wa Twitter, kuhusiana na ajali hiyo ambapo mabaki ya magari hayo yaliyohusika kwenye ajali yalisalia katika eneo la tukio, huku majeruhi wakipelekwa katika Hospitali za Nakuru Level Five na ile ya Molo Sub-County.
 


Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.