Viongozi na Wanachama wa chama cha mapinduzi ccm mkoani Tabora wameipongeza halmashauri kuu ya ccm Taifa kwa kukubali kuwapokea wanachama wapya waliojiunga na chama hicho hivi karibuni.







Na Mussa Mbeho,Tabora.

Viongozi na Wanachama wa chama cha mapinduzi ccm mkoani Tabora wameipongeza halmashauri kuu ya ccm Taifa kwa kukubali kuwapokea wanachama wapya  waliojiunga na chama hicho hivi karibuni.

Pongezi hizo zimetolewa  na baadhi ya viongozi na wanancham wa  ccm mkoani humo wakati wakizungumza na Mpandaradio  fm mara baada ya kikao cha halmashauri kuu ya ccm Taifa  kuwapokea wananchama wapya mapema hii leo Ikulu jijini Dareesalaam.

Athumani Mtunda na Mwamba Zuberi ni baadhi tu ya wananchama wa chama cha mapinduzi ccm mkoani humo wamesema wamefurahahi kuona viongozi hao wakirudi  ccm  kwa kuwa chama cha mapinduzi  ndio chama pekee chenye kuwaletea maendeleo watanzania.

Aidha wananchama hao wamewashauri viongozi wote wa vyama vya upinzani ambao bado hawajajiunga na chama cha mapinduzi ccm wajiunge na chama hicho   ili waweze kuchapa kazi kwa maendeleo ya Taifa.

Nae katibu wa jumuiya ya wazazi wilaya ya Tabora mjini Bi  Vaileth Lukas kasanga amesema kuwa chama cha mapinduzi ccm ni mzazi wa vyama vingine hivyo anawapongeza viongozi hao kwa kurejea ndani ya cham hicho huku akiwashauri kuwa na msimamo juu ya maamuzi yao .

Kwa upande wake katibu wa chama cha mapinduzi ccm wilaya ya Sikonge bwana Emanuel Alex amesema anawapongeza wananchama hao wapya kwa kujiunga na ccm huku akiwaomba wawe watulivu na kuchapa kazi kwa kumsaidia Rais Daktari John pombe joseph magufuri ili Tanzania iweze kusonga mbele kimaendeleo.

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.