Soko la Katumba Mnyaki linalomilikiwa na halamshauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi halina choo tangu kuanzishwa kwake miaka 40 iliyopita.



MPANDA 

Soko la Katumba Mnyaki linalomilikiwa na halamshauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi halina choo tangu kuanzishwa kwake miaka 40 iliyopita.

Hayo yamebainishwa na wakazi wa Kata ya Katumba wanaotumia soko hilo ambapo wamesema wanaishi kwa taharuki ya kukumbwa na kipindupindu kutokana na kukithiri kwa uchafu na ukosefu wa choo katika soko hilo.

INSERT…. WAKAZI KATUMBA

Baadhi ya wamiliki wa maduka ya kibiashara wamesema wanatozwa kuanzia shilingi elfu sita na mia tano huku wafanyabishara wanaouzia bidhaa chini wakilipa ushuru kila wanapouza lakini hawaoni jitihada zozote zikifanywa na mamlaka.

Kwa upande wao mwenyekiti wa soko hilo Bw.Leonard Kigwasu na Afisa Mtendaji wa vijiji vya Mnyaki A na B Bw.Kombo Masatu wamekiri kuwepo kwa uchafu sokoni hapo huku akisema choo kinatarajiwa kukamilika katika kipindi cha miezi miwili ijayo.

Source Isack Gerald

Editor Alinanuswe Edward

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.