RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA AVUNJA REKODI KATIKA AWAMU ZOTE KWA MSAMAHA WA WAFUNGWA WALIO HUKUMIWA KUNYONGWA






Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania  DK John Magufuli kwa mara ya kwanza katika historia ya taifa  amewasamehe wafungwa 61 waliokuwa wamehukumiwa kunyongwa.

Hata hivyo idadi ya wafungwa wengine walioachiwa huru kutokana na makossa mbali mbali ni 1,821 ambao amesema kuwa wanapaswa kuachiwa mara baada ya tangazo lake.

Miongoni mwa walio achiwa huru  ni mwanamuziki Nguza Viking na mwanawe Papii Kocha ambao walifungwa tangu 2004

Wafungwa wengine 8157 wamepunguziwa adhabu zao.

Idadi hiyo ya msamaha kwa wafungwa inatajwa kuwa ni kubwa katika awamu zote kuwahi kutokea na hasa zinazo wahusisha wafungwa wa kunyongwa na vifungo vya maisha


Maadhimisho  ya mwaka huu kauli mbiu yake ni ‘Uhuru Wetu ni Tunu, tuudumishe, Tulinde raslimali zetu, tuwe wazalendo, Tukemee rushwa na Uzembe, yanafanyika mjini hapa.’

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.