MKUU wa wilaya ya Sikonge Mkoani Tabora Peres Magiri amezindua wa ujenzi wa wodi mbili za wazazi






Na Mussa Mbeho,SIKONGE

MKUU wa wilaya ya Sikonge Mkoani Tabora Peres Magiri amezindua
wa ujenzi wa wodi mbili za wazazi katika kata ya kitunda ili kuweza kupunguza msongamano wa wagonjwa katika wodi ya akina mama wajawazito kwenye hospitali ya wilaya hiyo.


Akizungumza nara baada ya kuzindua ujenzi wa wodi hizo mkuu wa wilaya ya sikonge Bwana Peresi Magiri amesema  kuwa mpango wa ujenzi wa wodi hizo umeanzishwa ili kuboresha huduma za afya kwa mama na mtoto ikiwemo wajawazito na wagonjwa wengine wilayani humo.

Magiri  amesema Katika kuunga mkono jitihada za wananchi wa kata hiyo ofisi yake ya mkuu wa wilaya  itatoa  sh100,000/- ili kufanikisha ujenzi huo.

Nae Afisa Mtendaji wa kata hiyo bwana Ntegwa Machibula  amesema  ili kufanikisha ujenzi wa wodi hizo mbili na maabara ya somo la fizikia, viongozi na wananchi wa vijiji vyote wamekubaliana kwa pamoja kuchangia jumla ya sh. 34,155,000/- na zoezi la kukusanya michango hiyo bado linaendelea.


Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Kituo hicho Dk Mussa Maganga amepongeza hatua nzuri iliyochukuliwa na uongozi wa kata hiyo kwa kushirikianana serikali ya wilaya kwani itasaidia  kuboresha huduma za afya katika kituo hicho.

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.