MGOMBEA UENYEKITI JUMUIA YA VIJANA UVCCM MKOA WA KATAVI AKAMATWA NA KUACHIWA SAATANO USIKU



KATAVI



Uchaguzi wa jumuiya mbalimbali katika chama cha mapinduzi ccm mkoa wa katavi uliofanyika jana umeingia dosari kutokana na moja wa aliyekuwa mgombea wa nafasi ya uenyekiti UVCCM Benard Nswima kuenguliwa na kisha kukamatwa na polisi

Bwana Nswima alikamatwa na kisha kuachiliwa huru saa 5 usiku wa jana baada ya kuhoji kutoonekana kwa jina lake kwenye orodha ya wagombea ilhali alikwishapokea barua ya uteuzi kutoka katika ofisi yake

Katika utetezi wa sakata hilo Katibu wa UVCCM mkoa wa Katavi Bwana Abdulkarim G. Halamga amesema hatua ya kumtia nguvuni Bwana Nswima ilikuja ili kuzuia uchaguzi kutoharibika licha ya kukiri kuwa ni kweli Bwana Nswima anayo barua inayoonesha kuwa aliteuliwa kugombea kinyang’anyiro hicho

Uchaguzi huo wa Jumuiya ya Vijana UVCCM uliofanyika jana bwana Theonas Kinyonto ametangazwa kuwa mwenyekiti mpya huku bwana Dickson Kevilo akichaguliwa kuwa mjumbe wa mkutano mkuu UVCCM taifa

Katika nafasi zingine bi Feizal Shebidalla amechaguliwa kuwa mjumbe wa baraza kuu UVCCM na nafasi ya Mkutano mkuu amechaguliwa Bi Neema  Frank Tarimo

Source Haruna Juma

Editor Alinanuswe Edward

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.