Halmashauri ya Mpanda ya kanusha kitisho cha uwepo wa Pembejeo feki za kilimo






Halmashauri ya wilaya ya Mpanda mkoani Katavi imekanusha kuhusu uwepo wa pembejeo feki zinazo sambazwa na kutumika katika msimu huu wa kilimo.

Hayo yamesemwa na afisa kilimo wa halimashauri hiyo Bw Fabian Kashindye alipokuwa akizungumza na mpanda radio ambapo ameeleza kuwa kitisho hicho ni sawa na propaganda.

Zaidi ya asilimia 80 ya wananchi wa Tanzania hutegemea kilimo katika kuendesha maisha na kipato cha kaya, wengi wao ni kutoka vijijini ambao hukabiliwa na elimu duni kuhusu kilimo bora.


Hivi karibuni Waziri wa Kilimo, Dk Charles Tizeba ameitaja mikoa ya Rukwa, Njombe, Iringa, Songwe na Mbeya kuongoza kwa kuuza mbegu feki za mahindi na kusababisha madhara makubwa kwa wakulima, ikiwemo uzalishaji mdogo wa zao hilo

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.