MAREKANI YATAKA UTURIVU IRAQ


Wanajeshi wa Iraq wakishangiria Ushindi
Marekani imeombakuwepo utulivu baada ya wanajeshi wa serikali ya Iraq kuteka mji wa Kaskazini mwa Iraq wa Kirkuk na vituo muhimu kutoka kwa wakurdi.
Msemaji wa wizara ya mambo ya ndani Heather Nauert amezitaka penda zote kuzuia makabiliano zaidi.
Wanajeshi wa Iraq walielekea Kirkuk wiki tatu zilizopita, baada ya eneo la Kurdistan kuandaa kura ya maoni ya uhuru iliyokumbwa na utata.
Lengo lao ni kuteka sehemu zilizo chini ya udhibiti wa wakurdi tangu Islamic State wadhibiti eneo hilo.
Wenyeji wa maeneo yaliyo chini ya udhibiti wa wakurdi ukiwemo mji wa Kirkuk, kwa wingi waliunga mkono kujitenga kutoka Iraq wakati wa kura ya tarehe 25 mwezi Septemba.

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.