MANISPAA YA MPANDA KUANZA KUAJILI WATENDAJI WA KATA WA MUDA



Mkurugenzi mtendaji wa Manispaa ya Mpanda Michael Nzyungu ameagiza kuajiriwa kwa baadhi ya maafisa kata wa muda katika baadhi ya Kata.

Amesema hayo katika kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika jana katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda alipokuwa akijibu baadhi ya maswali yaliyo ulizwa na Waheshimiwa madiwani kuhusu tatizo hilo.

Katika hatua nyingine amezitaja baadhi ya sababu zilizopelekea upungufu wa watendaji hao kuwa ni baadhi yao kukumbwa na sakata la watumishi wenye vyeti feki.

Baraza la Madiwani linaendelea leo ambapo Madiwani watawasilisha mapendekezo mbali mbali ya utekelezwaji wa bajeti katika kata zao.


Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.