KESI YA KULIWA KWA KANUMBA KUANZA TENA




Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es salaam inatarajia kuanza kusikiliza ushahidi wa kesi ya mauaji bila kukusudia inayomkabili Msanii wa filamu nchini Tanzania, Elizabeth Michael maarufu kama ‘Lulu’.

Kwa mujibu wa ratiba ya vikao vya kesi za mauaji ya bila kukusudia iliyotolewa na Mahakama Kuu, kesi ya Lulu itaanza kusikilizwa siku ya Oktoba 19/2017 mbele ya Jaji Sam Rumanyika.
Lulu anakabiliwa na kesi hiyo akidaiwa kumuua Msanii mwenzake, Steven Kanumba bila kukusudia kinyume cha kifungu cha 195 cha kanuni za adhabu (PC), April 7/2012 nyumbani kwa marehemu Kanumba, Sinza Vatican.
Lulu na Kanumba walidaiwa kuwa ni wapenzi ambao mapenzi yao yalikuwa na siri kubwa mpaka tukio la kifo lilipomkuta Kanumba ndipo ilipofahamika juu ya mahusiano yao. 

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.