CCM SINGIDA YAMJIBU NYALANDU



Singida.
 Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida kimesema sababu zilizotolewa na aliyekuwa Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu za kuacha ubunge hazina mashiko, isipokuwa kilichomsukuma kufukia uamuzi huo ni hasira za kukosa uwaziri.
Katibu wa CCM mkoani Singida, Jamson Mhagama alisema jana Jumatatu Oktoba 30,2017 kuwa, “Kwa maono yake ameona siasa za nchi haziendi vizuri na kuamua kwenda kusaka siasa zitakazompendeza, tunamtakia kila la kheri. Ila tunamwonya kuwa asitarajie tena kupata ubunge kupitia Chadema anakolilia kwenda, CCM itashinda kwa kishindo katika uchaguzi mdogo ujao,” alisema.

“Wananchi walimwamini Nyalandu katika vipindi vyote vinne kwa kumpa kura za kutosha za nafasi ya ubunge. Kupitia kura hizo, Nyalandu amesifika na kujulikana kila kona sasa ameamua kuwapa kisogo wakazi wa jimbo la Singida Kaskazini, jina lake linaenda kufutika na hatasikika tena,” amesema Mhagama.

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.