MATOKEO YA UCHAGUZI KENYA YA FUTWA.





Mahakama yafuta matokeo ya uchaguzi wa urais Kenya
MOJA KWA MOJA
Mahakama ya Juu nchini Kenya imefutilia mbali matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika mapema mwezi uliopita katika uamuzi kuhusu kesi iliwasilishwa na muungano wa upinzani National Super Alliance.

UHURU KINYATA
RAILA ODINGA

Rais Uhuru Kenyatta alitangazwa mshindi wa uchaguzi huo akiwa na kura 8,203,290 (54.27%)

Tume ya uchaguzi ilisema Raila Odinga alipata kura 6,762,224 (44.74%)

Upinzani unadai mitambo ya tume ya uchaguzi ilidukuliwa na kuingiliwa kumfaa Rais Kenyatta.

Wakati wa kusikizwa kwa kesi, kulikuwa na mvutano kuhusu kukaguliwa kwa mitambo ya tume ya uchaguzi

Mahakama ya Juu inaweza kuidhinisha au kufutilia mbali matokeo ya uchaguzi.

Iwapo ushindi wa Rais Kenyatta utaishinishwa, basi ataapishwa Septemba 12


Iwapo uchaguzi utafutiliwa mbali, uchaguzi mwingine utafanyika katika kipindi cha siku 60.



Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.