KAULI ZA MAREKANI ZINANISHAUWISHI KUTENGENEZA SIRAHA ZAIDI....


Kim Jong-un amesema kauli za "wazimu'' rais wa Marekani Donald Trump zimemshawishi kuwa alikuwa sahihi kutengeneza silaha kwa ajili ya Korea kaskazini.
Katika kauli yake binafsi ambayo haikutarajiwa, kupitia vyombo vya habari vya taifa, Bwana Kim alisema kuwa Bwana Trump ''atalipia" hotuba yake ya hivi karibuni katika Umoja wa Mataifa.
Jumanne wiki hii rais wa Marekani alisema kwamba kama Marekani ikilazimishwa kujilinda ''itaiangamiza kabisa'' Korea Kaskazini.
Bwana Trump pia alimkejeli Bwana Kim akimuita "rocket man" anae andaa mpango wa ''kujiangamiza ".
Korea Kaskazini imekuwa ikifanya majaribio ya makombora, na ilifanya jaribio la sita la nuklia licha ya majaribio hayo kulaaniwa kimataifa.

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.