HATIMA YA WANAFUNZI WA DARASA LA SABA KATIKA SHULE YA MSINGI NSANDA ILIYOFUTWA KUJULIKANA.

Waliokuwa wanafunzi  10 wa darasa la saba katika  shule ya Msingi  Nsanda kata ya Kanoge halmashauri ya Nsimbo mkoani Katavi  iliyofungwa kwa madai ya kuwa katika hifadhi ya misitu watafanya mtihani wa darasa la saba katika shule ya msingi Kabuga.

Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nsimbo Filimbi Dipilo alipokuwa akizungumza na mpanda radio fm kuhusu hatima ya wanafunzi hao, ambapo amesema mkakati wa maandalizi ume kamilika na kwamba hakuna mwanafunzi atakaye shindwa kufanya mtihani huo.

Lakini ni takribani mwezi mmoja wanafunzi , hao wanaishi chini ya miti na wazazi  familia zao huku wakilalamika kupoteza daftari, na vitendea kazi vingine wakati wa operesheni ya kuondoa makazi katika maeneo hayo.

Kijiji cha Nsanda kipo Kaskazini mwa mkoa wa Katavi umbali wa KM 45 kutoka mji wa Mpanda ambapo wakazi walihamishwa kinguvu ikiwemo kuchomwa moto kwa makazi yao kwa kile kinachodaiwa kuwa ni eneo la hifadhi ya misitu.

Na Alinanuswe Edward.

Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.