Imebainika kuwa Wazazi na Walezi mkoani Katavi ni chanzo cha uwepo wa ndoa nyingi katika umri mdogo.
Hayo yamebainishwa na mwangalizi na mtetezi wa haki za binadamu kwa mikoa ya Katavi na Tabora Kusundwa Wamarwa alipokuwa akizungumza na Mpanda radio fm amesema suala hilo limeshamiri zaidi vijijini.

Aidha ameongeza kusema kuwa upo mpango wa kuendelea kutoa elimu ya malezi katika ngazi ya familia kwa kushirikiana na  jeshi la Polisi kupitia kitengo cha Dawati la jinsia na watoto pamoja na kamati za vijiji.
Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) imesema mkoa wa Katavi ndio unaoongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya wasichana wanaopata mimba wakiwa na umri mdogo  kwa asilimia 36.8, mikoa mingine ni Tabora 36.5 na Simiyu 32.1 huku Dar es Salaam ukiwa mwishoni kwa asilimia 12.
.





Comments

Popular posts from this blog

SAKATA LA KATA YA KATUMBA HALMASHAURI YA NSIMBO MKOANI KATAVI KUKOSA DIWANI LAIBUA MJADALA MPANA

MATOKEO YA DARASA LA SABA SHULE ZA SERIKALI CHALI

Wanawake wa kijiji cha Kabuga kata ya Kanoge Wilayani Mpanda/Katavi wamewalaumu viongozi kwa ahadi hewa.